Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Kamati ya Taifa ya Uongozi yatembelea walengwa Wilayani Babati Mkoani Manyara


Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF wakiwasikiliza Walengwa wa Mpango walipokuwa wakitoa ushuhuda wa mafanikio yao katika Kijiji cha Minjingu Wilayani Babati.

 

 

 Bi Elisifa el-Sangau akitoa ushuhuda mbele ya Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF jinsi  alivyofanikiwa kwa kutumia ruzuku ya itolewayo na TASAF Kusomesha Watoto, Kuboresha Makazi, Kujiunga kwenye Kikundi cha Kuweka Akiba na Kukopa pamoja na kuanzisha biashara ya  kusuka vikapu kutoka Kijiji cha Minjingu Wilayani Babati.

 

 

Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF wakiongozwa na kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw Charles Mwamaja kununua bidhaa zilizotengenezwa na walengwa kutoka Kijiji cha Minjingu Wilayani Babati

 

 

Walengwa wa Mpango wa  Kunusuru  Kaya za Walengwa wakimsikiliza Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF Bw Charles Mwamaj huku wakiendelea kusuka vikapu na mikeka katika Kijiji cha Minjingu Wilayani Babati

 

 

Bw Sifaeli Lengaramu akielezezaa mafanikio yake kwa kufuga kuku, mbuzi na ngombe mbele ya Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF 

 

 

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF Bw Charles Mwamaja, akimkabidhi fedha shilingi laki sita (600,000/-) Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya  Wilaya ya Babati Bi Anna Mbogo, zilizotolewa na wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Uongozi ya TASAF kwa ajili ya kukuza mitaji kwa vikundi sita vya walengwa wa TASAF vya kuweka Akiba na kukopa vya Kijiji cha Minjingu Wilayani Babati, kila kikundi kitapata shilingi laki moja.