Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu
Kipindi cha Pili cha TASAF Awamu ya Tatu Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ni cha miaka minne kuanzia 2020 – 2023. KIpindi hiki kinatekelezwa katika Mamlaka za Utekelezaji 187, ambazo ni halmashauri zote za Tanzania Bara, Unguja na Pemba. Mpango unatekelezwa katika Vijiji/Mitaa/Shehia zote nchini. Walngwa wa Mpango katika kipindi hiki ni kaya milioni moja na laki nne zenye watu wanaokadiriwa kuwa milioni saba.
Madhumuni ya Kipindi cha Pili ni kuongezafursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa na kulinda maslahi ya watoto wao.
Kipindi cha Pili kitafikia malengo yake kwa kutekeleza shughuli mbali mbali kupitia sehemu kuu tatu ambazo ni uhawilishaji fedha ambao utaongeza kipato cha kaya na kuwekeza katika afya na elimu ya watoto, kuinua uchumi wa kaya kwa kujenga uwezo kwa kaya katika utunzaji rasilimali na kutengeneza njia mbadala na endelevu za ajira na kushiriki katika kazi za jamii na kupata kipato cha ziada kwa matumizi ya kaya kama chakula na kugharamia mahitaji mengine ya msingi na wakati huo wakiboresha miundombinu katika jamii na kupata ujuzi na stadi za maisha.