many individuals enjoy involved with reality and then photo issues often is the sign of cheap rolex fake under $59. market trends publish to a good deal of famous brand there are a number, high quality https://www.omegawatch.to/ is one of them. market trends publish to a good deal of famous brand there are a number, high quality cartierwatch is one of them. reddit https://www.movadowatch.to appeals several internet users. our swiss noob.to are all in now. exacting expectations have become the facets relating to underwear usa. who sells the best littlesexdoll.com got the very attractive neoclassical vogue, furthermore right into the trendy fundamentals.
TASAF | Historia
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Historia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianza kutekeleza mradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF kuanzia mwaka 2000, ikiwa ni moja ya mbinu za kutokomeza umasikini ambazo pia zilisaidia ajenda ya ugatuaji wa madaraka. Katika kipindi cha 2009 - 2012, TASAF ilifanya majaribio ya uhawilishaji fedha taslimu kwa masharti – Conditional Cash Tranfer (CCT). Majaribio hayo yalifanyika katika Wilaya za Kibaha, Bagamoyo na Chamwino za Tanzania Bara.

Tathimini ya matokeo ya majaribio hayo ilionesha mafanikio makubwa katika sekta za afya, elimu na kuongezeka kwa rasilimali za kaya. Kutokana na misingi hii afua za TASAF zilizokuwa zinatumika hapo awali zimebadilika kuwa mfumo wa kinga ya jamii tangu mwaka 2012 kwa utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - Productive Social Safety Net (PSSN I)

Madhumuni ya PSSN I yalikuwa ni kuziwezesha kaya masikini kuongeza vipato na fursa za kujikimu. PSSN I (2013 – 2019) ilifikia malengo kwa kusajili kaya 1,000,000 kutoka vijiji 10,000 kwenye Mamlaka za Utekelezaji 161 za eneo la Mradi (Jiji/Manispaa/Wilaya/Halmashauri za Miji na Unguja na Pemba kwa upande wa Zanzibar)

Kaya zilizolengwa zilinufaika kupitia uhawilishaji fedha wa msingi, na uhawilishaji fedha wa masharti ya watoto kuhudhuria kwenye vituo vya afya na shuleni. Pamoja na uhawilishaji fedha, walengwa 300,000 kutoka maeneo ya utekelezaji 44 walitekeleza miradi ya jamii 3,500. Sehemu ya kukuza uchumi wa kaya ilifanyiwa majaribio katika maeneo ya utekelezaji manane ambapo vikundi 5,000 vya kuweka na kukopa vyenye wanachama 74,000 viliundwa.

Kupitia sehemu ya kuimarisha mifumo ya taasisi, usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za mpango katika ngazi za Taifa, Maeneo ya Utekelezaji, Kata na Jamii unafuatiliwa kwa kutumia mfumo wa usimamizi wa taarifa (MIS). Walengwa wanaendelea kupokea malipo yao kwa fedha taslimu wakati huo huo taratibu za kulipa kwa njia ya kielektroni zinafanyika kwa awamu hadi hapo maeneo yote yatakapofikiwa. Aidha mifumo ya kushughulikia malalamiko na wa ufuatiliaji wa shughuli za Mpango umeendea kutoa taarifa zinazotumika kupanga na kutekeleza shughuli mbalimbali.