Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Waziri Simbachawene Asifu Miradi ya TASAF Iringa


Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (MB) akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kinywang’anga Halmashauri ya Wilaya ya Iringa pamoja na wadau mbalimbali wa TASAF baada ya kukagua mradi wa Birika la kunyweshea mifugo lililojengwa kupitia Miradi ya Ajira za Muda inayotekelezwa na walengwa wa TASAF

Muonekano wa Mradi wa Birika la kunyweshea mifugo lililojengwa na TASAF katika Kijiji cha Kinywang’anga katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kupitia Miradi ya Ajira za Muda inayotekelezwa na Kaya za Walengwa

Ng’ombe wanaomilikiwa na Kaya mbalimbali za Walengwa katika Kijiji cha Kinywang’anga katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakinywa maji kwenye mradi uliojengwa na TASAF kupitia Miradi ya Ajira za Muda

Meneja wa Miradi ya Ajira za Muda na Uendelezaji wa Miundombinu wa TASAF Ndugu Paul Kijazi akitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi kwa Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (MB) alipotembelea Kijiji cha Kinywang’anga Halmashauri ya Wilaya ya Iringa