Habari
Miradi ya Sh bilioni 9 yatekelezwa Zanzibar

Miradi ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali 13 yenye thamani ya shilingi bilioni 9 imetekelezwa Unguja na Pemba kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa vituo vya afya, zahanati na ujenzi wa kumbi za mitihani katika shule.
Wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa ukumbi wa mitihani katika shule ya msingi na sekondari Bambi katika mkoa wa Kusini Unguja Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw Shedrack Mziray alisem a kuwa miradi hiyo itarahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw Shedrack Mziray akizungumza wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa ukumbi wa mitihani wa shule ya Msingi na Sekondari Bambi katika mkoa wa Kusini Unguja
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Tabia Mwitta Maulid alisema ujenzi wa ukumbi wa mitihani utaepusha msongamano wa wanafunzi wakati wa kufanya mitihani yao.
“TASAF inafanya kazi kubwa ya kujenga miundombinu mbalimbali na Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi hizi ambazo zinaleta manufaa kwa walengwa na jamii kwa ujumla,” alisema.
Waziri huyo aliwahimiza walengwa wa TASAF na wakazi wa Shehia ya Bambi kutoa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa mradi ambao unatarajiwa kukamilika Februari, 2024.
Katika ujenzi wa ukumbi huo, TASAF imetoa jumla ya shilingi million 117.5 ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 68.8 zimetumika na mradi umefikia asilimia 76
Jengo la ukumbi wa mitihani la shule ya msingi na sekondari Bambi