Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Simbachawene aweka jiwe la msingi ujenzi wa kituo cha afya Uzi


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Boniface Simbachawene ameweka Jiwe la Msingi kwenye Ujenzi wa Kituo cha Afya katika Shehia za Uzi iliyoko Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja. Uwekaji wa Jiwe la Msingi ikiwa ni mojawapo ya shamrashamra za Maadhimisho ya Miaka 59 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Boniface Simbachawene akisikiliza maelezo ya mchoro wa kituo cha afya kutoka kwa Mhandisi Ali Makame Ali

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga akielezea jinsi Mfuko huo ulivyoshiriki katika ukamilishaji wa ujenzi wa majengo ya Kituo hicho cha Afya

Waziri Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Pili ya Rais