Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango Azindua Kituo cha Afya Kendwa


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akifungua kitambaa kuashiria uzinduzi wa Kituo cha Afya Kendwa, Wilaya ya Mkoa wa Kusini Pemba. Uzinduzi wa kituo hicho cha Afya umefanyika katika shamrashamra za maadhimisho ya miaka 59 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha Afya Kendwa

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akikagua moja ya vyumba vya wauguzi wakati wa Uzinduzi wa Kituo cha Afya Kendwa

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga akitoa shukrani kwa viongozi na Wanakamati ya Usimamizi, Walengwa kwa ushiriki wao wa hali na mali katika kutekeleza ujenzi wa kituo hicho cha Afya

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi wa TASAF baada ya kuzindua kituo cha Afya kendwa