Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Wafanyakazi TASAF Wapata Mafunzo ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma Mahali pa Kazi


Wataalam kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wamefanya Mafunzo Juu ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma na Mahali pa Kazi kwa Watumishi wa TASAF yanayofanyika katika Ukumbi wa Antonia Maria Verna Hostel tarehe 24 hadi 26 mwezi wa kumi 2022 jijini Dodoma.

Mafunzo hayo yamefunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga na kuhudhuriwa na wafanyakazi wa TASAF wa kada mbalimbali.

Zifuatazo ni picha mbalimbali za matukio wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo:

 

Meneja wa Ufuatiliaji na Ushauri wa TASAF, Bi. Salome Mwakigomba (aliyesimama) akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga (katikati) ili kufungua Mafunzo ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma na Mahali pa Kazi kwa Watumishi wa TASAF

Meneja Rasilimali Watu wa TASAF, Bi. Mariam Al-Jabiri (aliyesimama) akiwakaribisha Watumishi wa TASAF kwenye Mafunzo ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma na Mahali pa Kazi

 

Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma na Mahali pa Kazi

 

Mafunzo ya Maadili na Mawasiliano kwa Umma na Mahali pa Kazi kwa watumishi wa TASAF yakiendelea katika Ukumbi wa Antonia Maria Verna Hostel Jijini Dodoma