the minutes and a sub-counter with the seconds. It is made of solid gold, but also their special styles bring a new echo to public and review modern ladies watches design. www.paneraireplica.co hublot replicas watches rolex deepsea replica The white lacquered dial in the upper right quarter of the watch features a blue minute track on the outside and printed roman numerals in black all around. replica iwcs breguet replica The Maurice Lacroix logo at 12 oclock is crisp and adds a finishing touch to the small dial. Just below the main dial is a small seconds indicator with another one of those bulky looking hands.

TASAF | Habari
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Walengwa wa TASAF Waaswa Kujiandaa Kuhitimu Kwenye Mpango


Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Steven Ndaki (aliyevaa kofia) akimsikiliza Bw. Allon Sanga ambaye ni mlengwa wa TASAF  katika maonesho ya Nane Nane yaliyofanyika Mkoani Mbeya

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Steven Mashauri Ndaki amewaasa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) kujiandaa kuhitimu kwenye Mpango huo na kuendelea na maisha ya kujitegemea bila kutegemea ruzuku baada ya kuwonekana wamefanya vizuri na kuwa imara kiuchumi. Bwana Ndaki aliyasema hayo wakati alipotembelea Banda la Maonesho la TASAF katika Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika Kitaifa katika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.

“Nawapongeza kwa hatua mliyofikia. Maelezo mliyonipa yanaonyesha kwamba mnwtumia vizuri ruzuku mliyopokea kujiimarisha kiuchumi na kutoka katika hali duni ambayo Mpango ulikuwa nayo, Naamini sasa mko tayari kuanza safari ya kujitegemea bila ruzuku ya TASAF. Anzeni maandalizi ya kuondoka kwenye Mpango na kuwapisha wengine wenye uhitaji mkiwa na mitaji ya kujiendeleza” alisema Bw. Ndaki

Naye Bi. Fasinesi Jatoni ambaye ni mlengwa kutoka katika mtaa wa Imbega kata ya Iziwa Jijini Mbeya alijinasibu kwa kusema kwamba TASAF imemnusuru kutoka katika umaskini wa kukosa hata mlo mmoja kwa siku na kumfikisha mahali ambapo anachagua aina gani ya vyakula ale yeye na kaya yake maana anavyo vingi mno.

“TASAF imeniheshimisha sana kiasi cha kunileta kwenye maonesho haya nikiwa na kuku chotara 17 ambapo kuku mmoja mdogo na tetea ninamuuza kwa shilingi 25,000  na hii imenipa hamasa sana ya kuendela na ufugaji hata baada ya kumalizika kwa maonesho haya” alisema Bi. Fasinesi.

Katika maonesho hayo, jumla ya wanufaika wa TASAF sita (06) kutoka katika vijiji na mitaa mbalimbali ya mkoa wa Mbeya wanashiriki wakiwa na bidhaa mbalimbali kama vile kuku, vikapu, mboga za majani, viazi mviringo, maziwa, vitunguu, pasheni, nyungo, ndizi na blokoli.