Habari
Ziara ya Wadau wa Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Tarehe 16 Juni, 2022

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw. Shauri Selenda, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa kwa wadau wa maendeleo walipomtembelea ofisini kwake (hawapo pichani)
Kiongozi wa Shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia nchini Tanzania, Bw. Michele Zini, akiuliza swali wakati wa ziara ya wadau wa maendeleo na maafisa wa TASAF baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa
Mkurugenzi wa Progamu za Jamii Bw. John Elisha (aliyesimama) akiwa na Wadau wa Maendeleo wakati wa mazungumzo na vikundi vya kuweka na kuwekeza katika kijiji cha Matimbwa, wilayani Bagamoyo
Kiongozi wa Shughuli za TASAF katika Benki ya Dunia nchini Tanzania, Bw. Michele Zini, (kulia) akiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na kikundi cha kuweka na kuwekeza Tupe Moyo wakati wa ziara ya wadau wa maendeleo katika kijiji cha Matimbwa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo
Wadau wa Maendeleo wakipata maelezo kutoka kwa Bi.Simwana Abdallah jinsi alivyojikwamua kiuchumi baada ya kupokea ruzuku ya uzalishaji mali katika kijiji cha Matimbwa, Wilayani Bagamoyo