Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Ikulu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii

Habari

Ziara ya Mafunzo kwa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa Zanzibar katika Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Bw. Shauri Selenda akikaribisha wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia ofisi ya viongozi wakuu wa kitaifa Zanzibar katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo

Mratibu wa TASAF Bagamoyo Bw. Jalala Sammatta akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa ngazi ya Halmashauri

Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza  la  Wawakilishi inayosimamia ofisi ya viongozi  wakuu wa kitaifa  Zanzibar Mhe. Machano Othman Said (katikati) akiwa katika  picha ya pamoja  na viongozi mbalimbali  katika  ofisi ya mkuu wa wilaya ya Bagamoyo

Mratibu wa TASAF Bagamoyo Bw. Jalala Sammatta akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia ofisi ya viongozi wakuu wa kitaifa Zanzibar kuhusu mradi wa kutengeneza matofali katika Shule ya Msingi Mwanamakupa kijiji cha Dunda Wilayani Bagamoyo

Wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia ofisi ya viongozi wakuu wa kitaifa Zanzibar wakiangalia bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na kikundi cha kuweka na kuwekeza cha Tupendane katika Kijiji cha Dunda Wilayani Bagamoyo

Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi  inayosimamia ofisi  ya viongozi  wakuu wa kitaifa  Zanzibar  Mhe. Machano Othman Said akizungumza na walengwa wa Mpango wa TASAF katika Kijiji cha Dunda Wilayani Bagamoyo

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash akizungumza na walengwa wa Mpango wa TASAF katika Kijiji cha Dunda Wilayani Bagamoyo

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Shedrack Mziray akizungumza na walengwa wa Mpango wa TASAF katika Kijiji cha Dunda Wilayani Bagamoyo